Search This Blog

Wednesday, December 21, 2022

MSAMBWANDA !!

 





    Mke wangu alisajili line mpya bila Mimi kujua,Jina lake Jenifa Godson.
    Jana usiku nimerudi home  akaniomba Tshs 10,000/= akasuke nywele nikamwambia sina ila nakupa Tshs 7,000/=
    Wakati tumelala,message ikaingia katika simu yangu "Hi,my Love!",Nikatoka nje(toilet) nikamjibu,"We ni nani?"
      MESSAGE:
    "Ni mimi Jen Msambwanda" kusikia sambwanda, Mshipa wa "Samsing" ukanicheza! 
        MIMI:
    Jen Msambwanda wa wapi tena?
       MESSAGE:
    "Buana baby,nawe,si pale unapokulaga kila siku?"                  
    MIMI:
    "Oooh,kumbe unaitwaga Jenifa!Namba yangu umeipata wapi?
      MESSAGE:
    Nimepewa na rafiki yako DJ Tipwili.
    Nakupenda sana handsome, sema huwa naogopaga kukwambia.Fahamu mi sijiwezi juu yako,yaani kila ukija kula, natamani usiondoke,nikwambie yaliyomo moyoni mwangu,Unanitesa mwenzio!" 
      MIMI:
    Ooh,Jamani pole mpenzi!
    Hata Mimi nilikuwa nakupenda,yaani kila nikiona hilo "tako",nahisi mzunguko wa damu ku-change! I love you too Honey!
        MESSAGE:
    Basi mpenzi,Nikuombe kitu?
      MIMI:
    Aaah,sema tu.
      Message:
    Naomba Tshs 50,000/-
       MIMI:
    Nakutumia sasa hivi.(Nikatuma)
       MESSAGE:
    Wow!
    Asante mume wangu,haya rudi ndani tulale.Ni mimi mkeo Mama Kiduku hapa!
    ‍♂‍♂‍♂
    Basi mwenzenu leo nimezuga zangu mlinzi nipo nje hata ndani sitaki kwanza hakuna hata feni  alafu mbu wengi Acha awake mwenyewe !

0 comments:

Post a Comment

BLOG