KATIKA
tawala ya MAPAMBANO palikuwa na walinzi 12 waliokuwa wakilinda ghara la chakula
ambacho wanannchi walikuwa wakikiifadhi pindi njaa itakapotokea basi watumie
chakula hicho.
Walinzi
hao walilinda ghala hilo kwa takribani miaka 10 wakipigana na wezi mbali mbali
pia na wavamizi mbalimbali kutoka tawala jirani waliotaka kuiba chakul a hicho
kwa manufaa yao.
Katika
walinzi hao 12 palikuwa na mlinzi mmoja mvutaji wa sigara.Siku moja wakiwa
wamengia lindo la usiku yapata majira ya saa 1 jioni waliingia ndani ya ghala
ili kuhakikisha kuwa chakula kipo salama.Wakati wanakagua yule mlinzi mvuta
sigara alikuwa anavuta sigara wakati huo.Mmoja kati ya walinzi wenzake
alimwambia"Zima sigara usije ukasababisha moto".Yule mlinzi alimjibu
mwenzake"Nipo makini siwezi kuunguza".
Wakati wanatoka mlangoni jivu la sigara lililokuwa na moto lilipepeluka na kutua kwenye gunia la chakula.Pasipo wao kujua walifunga ghala na kuanza kulinda.Usiku baada ya muda kidogo kupita wakiwa wamepitiwa na usingizi kidogo mmoja wa walinzi wale aliamka na kwa mshangao aliona moto mkubwa sana ukiteketeza ghala.Walipiga kelele hatimae wanannchi waliamka na kuanza kuuzima moto.Walifanikiwa kuuzima lakini nusu ya chakula ghalani kilikuwa kimeteketea.Msako wa nani aliesababisha moto ulianza na hatimae walinzi wenzake na yule mvuta sigara walimtaja mwenzao kuwa ndie chanzo kwa sababu aliingia na sigara mle ndani.
Wakati wanatoka mlangoni jivu la sigara lililokuwa na moto lilipepeluka na kutua kwenye gunia la chakula.Pasipo wao kujua walifunga ghala na kuanza kulinda.Usiku baada ya muda kidogo kupita wakiwa wamepitiwa na usingizi kidogo mmoja wa walinzi wale aliamka na kwa mshangao aliona moto mkubwa sana ukiteketeza ghala.Walipiga kelele hatimae wanannchi waliamka na kuanza kuuzima moto.Walifanikiwa kuuzima lakini nusu ya chakula ghalani kilikuwa kimeteketea.Msako wa nani aliesababisha moto ulianza na hatimae walinzi wenzake na yule mvuta sigara walimtaja mwenzao kuwa ndie chanzo kwa sababu aliingia na sigara mle ndani.
Wanannchi
wakiwa na hasira kali sana walimchukua yule mlinzi huku wakimpiga na kumdhihaki
kwa matusi kutokana na kusababisha hasara wakaamua kumpeleka mbele ya mfalme
akapate hukumu.Walipofika kwa mfalme kila mmoja alipiga kelele kuwa yule mlinzi
anatakiwa auwawe kwa sababu ya hasara aliyosababisha ya chakula.Mfalme
alimtazama yule mlinzi ambae nguo zake zimejaa damu kutokana na kipigo cha
wanannchi.Kisha akanyanyua macho yake pia kuwatazama wanannchi waliokuwa na
hasira wakisubiri hukumu ya mlinzi kuuawa.Mfalme alipokuwa akipepesa macho yake
kwa wanannchi mara alimuona mtoto mmoja mdogo mwenye miaka kama 10 akiwa pale
nae akisubiri hukumu ya yule mlinzi
Mfalme
alimfuata yule mtoto kisha akachuchumaa na kumpapasa mashavuni kisha akaagiza
vipanda vya fedha vyenye thamani kubwa viletwe.
Mfalme alimuuliza yule mtoto"Baba yako yuko wapi".Mtoto alinyoosha kidole kuonyesha baba yake alipo ambae nae alikuwa mmoja wa waandamanaji wa hukumu ya yule mlinzi.Mfalme aliamuru vile vipande vya fedha vyenye thamani kubwa apewe yule mtoto.
Mtoto alifurahi sana kuona kapewa fedha ambayo angeweza kununua kitu chochote kitamu akipendacho.Kisha mfalme akamuuliza tena yule mtoto"Kati ya mimi na baba yako unachagua kuishi na nani".Mtoto bila kupindisha maelezo na kwa sauti kubwa alisema anachagua kuishi na mfalme.
Mfalme alimuuliza yule mtoto"Baba yako yuko wapi".Mtoto alinyoosha kidole kuonyesha baba yake alipo ambae nae alikuwa mmoja wa waandamanaji wa hukumu ya yule mlinzi.Mfalme aliamuru vile vipande vya fedha vyenye thamani kubwa apewe yule mtoto.
Mtoto alifurahi sana kuona kapewa fedha ambayo angeweza kununua kitu chochote kitamu akipendacho.Kisha mfalme akamuuliza tena yule mtoto"Kati ya mimi na baba yako unachagua kuishi na nani".Mtoto bila kupindisha maelezo na kwa sauti kubwa alisema anachagua kuishi na mfalme.
Pale
pale mfalme alimgeukia yule baba wa mtoto na wanannchi kwa ujumla na kuanza
kuwapa somo."Angalieni nyinyi wenyewe mashahidi mtoto huyu amekaa na baba yake
zaidi ya miaka kumi.Baba yake amehangaika kumlisha na kumvisha mpaka kufikia
umri huo.Baba yake amepoteza mali na mali amepoteza usingizi na usingizi ili
mladi tu kumpigania mtoto huyu akue.Baba yake amehangaika kutafuta dawa pindi
mtoto huyu alipokuwa anaumwa,Alihangaika kumbembeleza pindi mtoto huyu alipokuwa
analia lakini cha ajabu leo nimempa vipande vichache vya fedha ambavyo havina
kabisa thamani yoyote ya gharama ambayo mzazi wake amemtuza mpaka kufikia hapa
lakini mtoto huyu ameniona mimi ni wadhamani kuliko hata mzazi wake aliemtuza
miaka 10 na kufikia hatua ya kumkana mzazi wake mbele ya umati wa watu na
kuchagua kuishi na mimi kisa kaona kapewa vipande vya fedha ambavyo angeweza
kununua chochote kitamu akipendacho."Mfalme aliendelea kusema."Ndivyo ilivyo leo
kwa mlinzi huyu ambae amelinda ghala lenu la chakula zaidi ya miaka 10 na
kupigana na wezi na majambazi wa kila aina kwa ajili ya kupigania chakula chenu
lakini leo kosa moja tu alilolifanya mnataka msahau mazuri yote ya miaka kumi
aliyoyafanya mlinzi huyu kama vile mtoto huyu alivyosahau mazuri yote ya mzazi
wake aliyotendewa kwa miaka kumi kisa vipande vya fedha vya siku moja.Je sisi ni
watu wa roho gani wa kupenda kukumbuka mabaya tu na kusahau
mazuri.?"
Taratibu wanannchi walianza kutupa mawe na siraha za kuulia walizokuwa wamebeba kwa ajili ya kumuuwa mlinzi huyo walianza kusogea nyuma kwa aibu na kujiona ni wakosaji sana.
Taratibu wanannchi walianza kutupa mawe na siraha za kuulia walizokuwa wamebeba kwa ajili ya kumuuwa mlinzi huyo walianza kusogea nyuma kwa aibu na kujiona ni wakosaji sana.
MFALME
alitoa mamlaka kuwa mlinzi yule hatouwawa na badala yake mfalme alimpandisha
cheo mlinzi yule na kuwa mkuu wa ulinzi katika nnchi yake na kumtahadhalisha awe
makini na kazi siku nyingine ili yasije yakamtokea mabaya zaidi ya
yale.
TURUDI
KATIKA JAMII YETU SISI
....MUDA
mwingine kwenye ndoa zetu,mtaani kwetu,au katika jamii yetu watu wamekuwa wepesi
sana wa kusahau yale mazuri machache machache tunayoyatenda.Badala yake wamekuwa
bora sana wa kuangalia kosa moja la bahati mbaya ulilolitenda na kukusema kila
sehemu mbaya zaidi wale uliokuwa nao karibu ndio wanakuwa watu wa kwanza
kukusema na kukudhihaki kama wenzake na huyo mlinzi.
Nauliza je katika jamii yako au hapo unapoishi watu wa hivi kama hawa wanannchi wa kwenye tawala ya MAPAMBANO hawapo??.
Mungu akusaidie sana kukuepusha mbali na hawa watu
AMEN.
Nauliza je katika jamii yako au hapo unapoishi watu wa hivi kama hawa wanannchi wa kwenye tawala ya MAPAMBANO hawapo??.
Mungu akusaidie sana kukuepusha mbali na hawa watu
AMEN.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment