.
Alikuwa bafuni akioga...
"Honey, mama yako anakupigia..anataka umtumie pesa uliyomwambia mapema" Mkewe akawa akimwambia mumewe huku akiwa chumbani
"Sawa wife, naomba nisaidie ingia kwenye menu ya M-PESA kwenye simu yangu na mtumie shilingi laki moja" Mume akaongea kwa nguvu kutoka bafuni.
Mke akastaajabu. Inakuaje kirahisi rahisi hivyo Mumewe anamuamini na account yake ya MPESA.
"Baby, simu yako umeweka password. Mimi sijui password yako" mke akashauti tena kumwambia mumewe aliyepo bafuni...
"Password ya simu ni 2789. Na passowrd ya MPESA ni hiyo hiyo 2789" Mume nae akamjibu mkewe kutokea bafuni..
Akachukua simu ya mumewe, akaingiza password 2789 na simu ikawa unlocked. Akamtumia mama mkwe wake shilingi laki moja kama alivyoambiwa na mumewe.
Baada ya kutuma, akaingiwa na tamaa ya kupitia pitia sms kwenye simu ya mumewe. Akajiuliza maswali, kwanini mumewe aweke Password kwenye simu yake? Anaficha nini?
Akiwa anaangalia angalia chats mbalimbali facebook, WhatsApp na sms za kawaida kwenye simu ya mumewe hakuamini macho yake...
Chats nyingi zilionesha mumewe akimzungumzia yeye vizuri kwa marafiki zake na familia yake, aliona sms nyingine mumewe akimsifia hata mbele ya wanawake wengine...
Mke akatabasamu na kujawa na uso wa furaha baada ya kuona mumewe kwa kiasi gani anamjali. Akaona ni kwa kiasi gani mumewe yupo upande wake akimpigania..
Akaona baadhi ya wanawake waliokuwa wakimtumua sms za kiuchokozi chokozi jinsi walivyomwagwa, na baadhi yao aliona mumewe amewatumia picha yao ya pamoja na kuandika caption kwamba "Huyu ndiyo mwanamke nimpendae" Kitu ambacho kiliwaziba midomo wanawake wengine..
Kadiri alivyozidi kupekua simu ya mumewe ndivyo alivyozidi kugundua ni kwa namna gani mumewe ni rafiki mzuri kwa watu. Anao marafiki wengi kwenye chat list yake na marafiki wa kweli wakizungumza dili za maana..anapendwa na wengi na wanamkubali..
...Akaona ni kwa kiasi gani mumewe anawaombea watu, akiwaandikia sala na akiwabariki..akaona sms za kuwatia moyo wale waliokuwa wakimuandikia issue zozote za ushauri..
...Huyu mume wake ni wa ajabu, mume muaminifu, rafiki wa kweli, ndugu mwajibikaji kwa ndugu na wazazi wake, na mzungumzaji mzuri ambapo watu wengi wanapenda kuongea na kuchat nae..
..Mke akajisikia vibaya kwa hapo mwanzo kuwaza kwamba mumewe sio muaminifu jambo ambalo si kweli.
"Umeshamtumia mama pesa?" Mumewe akamuuliza huku akitoka bafuni akiwa amejifunga taulo.
"Ndio babylove..njoo hapa mpenzi wangu" Mke akamwambia mumewe huku akiinuka kitandani na kuweka simu pembeni.
Akamkumbatia mumewe kwa nguvu..
Akambusu kwa hisia kali. Uaminifu unampa raha mwanamke.
Akamvua taulo mumewe. Akamsukuma kitandani na kuanza kukanda kanda mwili wa mumewe..
"Oh baby, inaonesha una njaa na mimi eeh" Mume akaongea huku akisikilizia raha ya kupapaswa na mikono laini ya mkewe jambo lilofanya hisia zake ziamke.
Mke akakaa juu ya mumewe na wakafanya lile tendo lililoidhinishwa kwao...naam tendo la ndoa.
"Nakupenda sana swewtheart" mke akamwambia mumewe baada ya kumaliza mtanange.
"Nakupenda pia Darling". Mume akamjibu mkewe huku akimbusu kwenye paji la uso.
Siku chache baadae, alipomuuliza mumewe kwanini ameweka password kwenye simu yake, mumewe alimjibu kuwa ameweka password kwa sababu ya usalama wa nyaraka zake na pia kulinda usiri wa zile chats hot ambazo wamekuwa wakichat pamoja kama mke na mume. Kwamba watu wengine wasipate kuona maongezi yao.
Mke akakumbuka mambo ya kikubwa waliyokuwa wakichat na mumewe hasa pale anapokua mbali nae na akaona mantiki ya mumewe kuweka password kwenye simu yake.
______________________________
Usiwe mwepesi sana kumhisi mpenzi wako vibaya. Sio kila mtu ni msaliti kwenye ndoa yake. Kuna watu wako serious na mahusiano yao. Kwa sababu usaliti ni maamuzi ya mtu binafsi na wala sio bahati mbaya.
"Cheating is hard work. You gotta keep deleting text, keep locking your phone, keep deleting messages off of facebook, twitter, whatsap and think of lies..that's too much! rather be loyal"
Blessed are you if you are a faithful spouse married to or having a faithful spouse...
MWISHO
0 comments:
Post a Comment