"Akiwa na miaka kumi na minane, Kijana Junior alianza kuzitambua shida alizokuwa akipitia mama yake,hii ni baada ya kumaliza darasa la saba na kukaa nyumbani kwa muda baada kukoswa hela za kuendelea na masomo yake ya elimu ya sekondari, hapo ndipo Junior alipomkalisha vizuri mama yake na kumhoji kuhusu baba yake, na haya ndo yalikuwa maelezo ya mama Junior alipomsimulia mwanae"
"Mwanangu,, Baba yako alinipa ujauzito baada ya kumaliza darasa la saba, baada ya kuligundua hilo nilimfuata na kumuambia ukweli alikataa japokuwa alikuwa anajua kuwa muda mwingi aliutumia kuwa na mimi,, ilipita wiki moja tu nikasikia amefunga ndoa na mwanamke mwingine, ni kitu kilichoniuma haswa na huwa kinaniuma mno katika maisha yangu kila ninapokumbuka,,
**************
"Mimba yangu ilizidi kuwa kubwa sana, nilijitahidi kujihudumia mwenyewe kwakuwa bibi yako hakuwa na uwezo hata kidogo maana kila nilipokuwa namfuata baba yako kumuomba hela alikuwa ananifukuza na ninapopiga simu yake alikuwa akimpa mwanamke wake anapokea simu yangu, nilijaribu kuuliza kwanini kanifanyia hivyo, nikabaini kuwa alikuwa ananitumia tu kwa starehe zake kwani alikuwa na mwanamke mwingine pembeni, pia alikuwa akiwaambia marafiki zake kuwa hawezi kunioa mimi mtoto wa maskini ataoa tajiri mwenzie, kingine kinachonifanya hata nisitamani kuolewa na mwanaume mwingine, wakati nakuzaa wewe nilijifungua kwa shida sana kwani nilifanyiwa upasuaji na kutolewa mfuko wa uzazi, kwahiyo siwezi kuzaa tena, na hakuna mwanaume ambaye atakubali kuoa mwanamke ambaye hatamzalia mtoto,, sikutaka kukwambia yote haya kwakuwa sikutaka umchukie baba yako.... Yote kwa yote usimchukie baba yako kwani bado ni baba yako tu.
Alizungumza mama Junior, wakati huo wote Junior alikuwa kimya kabisa akimsikiliza mama yake kwa makini kwani alikuwa akiongea huku analia na kumfanya Junior naye ashindwe kuvumilia na kujikuta akidondosha machozi...
*********************
"Junior alishusha pumzi nzito huku akiinuka na kumsogelea mama yake akaanza kumfuta machozi na kumbembeleza hadi aliponyamaza,,
"Usijali mama yangu kuhusu mimi kusoma, najua kuna matajiri wengi Duniani ambao hawajasoma, hivyo nami nitakuwa tajiri siku moja na nitakuja kukutunza pia"
Alizungumza Junior huku akimuachia mama yake na kuingia chumbani kwake na kuanza kupangapanga nguo zake,,,,
*******************
"Hatimae kulipambazuka,Junior aliamka asubuhi sana siku hiyo na kubeba begi dogo lililokuwa na nguo na kuanza safari,, kwakuwa hakuwa na hela yoyote alitembea kwa mguu kutoka Sengerema hadi kamanga, alipofika hapo alishindwa kuendelea na safari yake kwani hakuwa na hela ya kukata ticket kwa ajiri ya kuvuka,,kwakuwa usiku nao tayari ulikuwa umeshakuwa mkubwa, hatimae aliamua kutafuta sehemu ya kulala, alifungua begi lake na kuchukua shuka lake na kujifunika huku usingizi mkubwa ukimchukua,,
"Alikuja kushtuka usiku sana baada ya baridi kali sana kumpiga, alishangaa alipojikuta akiwa na nguo alizokuwa amevaa tu, hapakuwa na begi wala shuka alilokuwa amejifunika, bila shaka vibaka walikuwa wamepita navyo, Baridi ilizidi kuwa kali sana kiasi cha kumkosesha usingizi kabisa Junior, alianza kumkumbuka mama yake na kuanza kujilaumu kwa kuondoka bila kumuagaa, wakati anawaza hayo aliona moto umbali kidogo na alipokuwa akajikuta akitamani kuupata, alianza kupiga hatua hadi alipoukaribia, alishangaa kukuta kijana mmoja tu akiwa amekaa huku akianika nguo zake zilizokuwa mbichi muda huo, Junior aliangalia pembeni akaona mtumbwi mdogo, bila shaka jamaa yule alikuwa ametoka ziwani kùvua, Junior alimsalimia jamaa yule akaitikia huku akimkaribisha Junior kwani alizani mvuvi mwenzie...
********************
"Junior aliutumia muda huo kuusogelea moto ule na kuanza kupiga story mbili tatu na yule jamaa ambaye alionekana kuwa mchangamfu sana.,
"BHEBHE NGALU, MISHAGA WELAGHA"
"Ni Sauti iliyomshtua Junior kutoka usingizini ikimtaka kuamka, Junior hakuwa na jinsi aliamka japo giza bado lilikuwa limetanda juu ya anga, bila shaka ilikuwa saa tisa au kumi usiku..
**********************
"Twende ukanisaidie kuvuta nyavu rafiki yangu, si unajua nipo peke yangu baada ya wenzangu kuzama,, kwahiyo boss wangu hadi atafute vijana wengine tena napata shida sana kufanya hii kazi peke yangu"
alizungumza Jamaa yule na kumfanya Junior kuingiwa na uwoga kidogo kwani alikuwa hajawahi kufanya kazi hiyo ila hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali
"Waliingia ndani ya mtumbwi na kuanza kukata mawimbi hadi ziwani, Junior ilibidi awe mkweli, alimwambia jamaa yule kuwa ndo mara yake ya kwanza, jamaa akatabasamu kidogo,
"Hata mimi nilijifunza, hebu niangalie mimi ninavyofanya nawewe ujaribu"
Alizungumza jamaa yule na kumfanya Junior kuangalia kwa makini, ndani ya dakika kadhaa Junia alikuwa ameshajua na kuanza kumsaidia yule jamaa, Mungu si Athumani wala Dossa,, siku hiyo walipata samaki wengi sana hadi yule jamaa akashangaa, Asubuhi wakaenda kukabidhi wale samaki kwa boss wao ambaye naye alishangaa sana kwani mzigo siku hiyo ulikuwa mkubwa sana zaidi ya siku zote, na kwakuwa hapakuwa na wafanyakazi wengi ilikuwa ni rahisi kwa Junior kuajiriwa na kampuni ile iliyokuwa inasimamiwa na mzungu,,,
*****************************
"Ilipita wiki moja Junior tayri alikuwa mvuvi hodari sana kitendo kilichomfahisha sana boss wake na kuzidi kumsifikia huku akimuahidi kumuongezea mshahara wake, muda wote huo Junior hakuweza kuwasiliana na mama yake ambaye alitafuta hadi akakata tamaa na kuzidi kuchanganyikiwa akajikuta analazwa hospital, mwezi ulipita na Junior kupewa mshahara wake wa kwanza, siku alipopokea mshahara cha kwanza alinunua simu na namba ya kwanza kuisave ilikuwa ni namba ya mama yake,,baada ya kuisave alijaza vocha na kuipigia namba ile, mama yake alipokea kwa kuuliza nani mwenzangu huku sauti yake ikiwa imechoka sana,,
"Ni Mimi mwanao Junior mama"
baada ya sauti ile,alisikia vigeregere vya mama yake na kuwafanya hadi waliokuwa wanamhudumia kushangaa kwani mama Junior alipona ghafla, shangwe zile zilimfanya Junior kuamini kuwa mama yake anampenda mno na ndo pekee anayemtegemea maishani mwake,waliongea mengi sana huku akimtumia mama yake nusu ya mshahara wake"
"Siku zilizidi kwenda huku Junior akiendelea kugawana na mama yake mshahara hivyohivyo,, miaka ilisogea huku Junior akipandishwa kazi na kukabidhiwa ofisi yake kutokana na uaminifu wake kazini na utendaji kazi wake"
"Siku moja Junior akiwa ndani ya gari yake mpya aliyokuwa amenunua akirudi nyumbani kwao, alishangaa akisinamishwa na mzee mmoja aliyekuwa akitembea kwa mguu huku akiwa amepauka sana na kumuomba lift kwani nae alikuwa anaenda Sengerema, Junior hakuwa na kutu moyoni mwake,alimpa lift mzee yule na kuanza kupiga nae story moja mbili,,mzee yule alijikuta akifunguka na kumsimlia maisha aliyopitia;
"Kijana wangu, wakati nikiwa kijana kama wewe nilioa mwanamke ambaye alikuwa mtoto wa kitajili haswa, wazazi wake walitupa kila kitu hadi kazi pia walinipa,nimeishi na mwanamke yule bahati mbaya nikaugua tezi Fulani ya kizazi,madaktari wakaniambia sitakuwa na uwezo wa kumbebesha mimba mwanamke,, kilichoniuma zaidi ilipita miaka miwili nikaona mke wangu tumbo limejaa,nilipomuuliza akanijibu kwa dharau kuwa hawezi kuishi na mwanaume suluari,kiukweli niliumia sana nikaamua kumuacha ila ndo hivyo sikutoka na kitu kwani mali zote zilikuwa za mwanamke,niliingia mjini na kuanza kutafuta kazi lakini sikupata kazi ya maana zaidi ya kazi ndogondogo za kunipatia chakula,, kwa sasa nimezeeka nimeona nirudi nyumbani nikafie kwenye mashamba ya wazazi wangu kwani hapa nilipo nina kansa pia na siku zangu za kuishi zinahesabika,nani atanizika huko mjini wakati sina ndugu hata mmoja,bora hata ningekuwa na watoto"
alizungumza mzee yule nakumfanya Junior kutokwa na machozi kwani aliikumbuka simulizi ya mama yake,
"ukimya ulitawala kwa muda hatimae Junior akafanikiwa kufika mbele ya nyumba fulani ambayo ndo kwanza ilikuwa imekamilika, alisimamisha gari na kushuka, wakati huo mama yake alikuwa jikoni, alipomuona mwanae alikimbia kwa furaha na kumkumbatia huku akishangaa gari ilivyokuwa inang'aa, wakati anashangaa ile gari mara aliona mtu akishuka,,,
"karibu mzee huyu ndo mama yangu"
alizungumza Junior ila alishangaa mzee yule akiwa amemkodolea macho mama junior wakati huo mama junior nae akiwa amemtolea macho mzee yule
"Junior baba yako huyooooo"
alipiga kelele mama junior wakati huo yule mzee alimwangalia mama Junior
"Sarah huyu ndo mwanangu,nisamehee mama"
baada ya kutamka maneno yale yule mzee alianguka hapohapo, Junior aliwahi akambeba na kumuingiza ndani ya gari na kumpeleka hospital, alikaa nje na mama yake wakiwa na hamu ya kujua maendeleo ya baba yake ambaye siku zote alikuwa anatamani kumfaham, baada ya muda waliitwa na dokta,,,,
"Kwanza niwape pole, kiukweli mgonjwa wenu hatuko naye tena duniani kwani ameugua kansa kwa muda mrefu sana ambayo imeathiri mapafu,bora mngemuwahisha ingesaidia"
Junior alilia sana baada ya majibu Yale, siku ya kwanza kumfahamu baba yake,ndo siku baba yake anafariki,,,,,,,,
**************
"Mimba yangu ilizidi kuwa kubwa sana, nilijitahidi kujihudumia mwenyewe kwakuwa bibi yako hakuwa na uwezo hata kidogo maana kila nilipokuwa namfuata baba yako kumuomba hela alikuwa ananifukuza na ninapopiga simu yake alikuwa akimpa mwanamke wake anapokea simu yangu, nilijaribu kuuliza kwanini kanifanyia hivyo, nikabaini kuwa alikuwa ananitumia tu kwa starehe zake kwani alikuwa na mwanamke mwingine pembeni, pia alikuwa akiwaambia marafiki zake kuwa hawezi kunioa mimi mtoto wa maskini ataoa tajiri mwenzie, kingine kinachonifanya hata nisitamani kuolewa na mwanaume mwingine, wakati nakuzaa wewe nilijifungua kwa shida sana kwani nilifanyiwa upasuaji na kutolewa mfuko wa uzazi, kwahiyo siwezi kuzaa tena, na hakuna mwanaume ambaye atakubali kuoa mwanamke ambaye hatamzalia mtoto,, sikutaka kukwambia yote haya kwakuwa sikutaka umchukie baba yako.... Yote kwa yote usimchukie baba yako kwani bado ni baba yako tu.
Alizungumza mama Junior, wakati huo wote Junior alikuwa kimya kabisa akimsikiliza mama yake kwa makini kwani alikuwa akiongea huku analia na kumfanya Junior naye ashindwe kuvumilia na kujikuta akidondosha machozi...
*********************
"Junior alishusha pumzi nzito huku akiinuka na kumsogelea mama yake akaanza kumfuta machozi na kumbembeleza hadi aliponyamaza,,
"Usijali mama yangu kuhusu mimi kusoma, najua kuna matajiri wengi Duniani ambao hawajasoma, hivyo nami nitakuwa tajiri siku moja na nitakuja kukutunza pia"
Alizungumza Junior huku akimuachia mama yake na kuingia chumbani kwake na kuanza kupangapanga nguo zake,,,,
*******************
"Hatimae kulipambazuka,Junior aliamka asubuhi sana siku hiyo na kubeba begi dogo lililokuwa na nguo na kuanza safari,, kwakuwa hakuwa na hela yoyote alitembea kwa mguu kutoka Sengerema hadi kamanga, alipofika hapo alishindwa kuendelea na safari yake kwani hakuwa na hela ya kukata ticket kwa ajiri ya kuvuka,,kwakuwa usiku nao tayari ulikuwa umeshakuwa mkubwa, hatimae aliamua kutafuta sehemu ya kulala, alifungua begi lake na kuchukua shuka lake na kujifunika huku usingizi mkubwa ukimchukua,,
"Alikuja kushtuka usiku sana baada ya baridi kali sana kumpiga, alishangaa alipojikuta akiwa na nguo alizokuwa amevaa tu, hapakuwa na begi wala shuka alilokuwa amejifunika, bila shaka vibaka walikuwa wamepita navyo, Baridi ilizidi kuwa kali sana kiasi cha kumkosesha usingizi kabisa Junior, alianza kumkumbuka mama yake na kuanza kujilaumu kwa kuondoka bila kumuagaa, wakati anawaza hayo aliona moto umbali kidogo na alipokuwa akajikuta akitamani kuupata, alianza kupiga hatua hadi alipoukaribia, alishangaa kukuta kijana mmoja tu akiwa amekaa huku akianika nguo zake zilizokuwa mbichi muda huo, Junior aliangalia pembeni akaona mtumbwi mdogo, bila shaka jamaa yule alikuwa ametoka ziwani kùvua, Junior alimsalimia jamaa yule akaitikia huku akimkaribisha Junior kwani alizani mvuvi mwenzie...
********************
"Junior aliutumia muda huo kuusogelea moto ule na kuanza kupiga story mbili tatu na yule jamaa ambaye alionekana kuwa mchangamfu sana.,
"BHEBHE NGALU, MISHAGA WELAGHA"
"Ni Sauti iliyomshtua Junior kutoka usingizini ikimtaka kuamka, Junior hakuwa na jinsi aliamka japo giza bado lilikuwa limetanda juu ya anga, bila shaka ilikuwa saa tisa au kumi usiku..
**********************
"Twende ukanisaidie kuvuta nyavu rafiki yangu, si unajua nipo peke yangu baada ya wenzangu kuzama,, kwahiyo boss wangu hadi atafute vijana wengine tena napata shida sana kufanya hii kazi peke yangu"
alizungumza Jamaa yule na kumfanya Junior kuingiwa na uwoga kidogo kwani alikuwa hajawahi kufanya kazi hiyo ila hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali
"Waliingia ndani ya mtumbwi na kuanza kukata mawimbi hadi ziwani, Junior ilibidi awe mkweli, alimwambia jamaa yule kuwa ndo mara yake ya kwanza, jamaa akatabasamu kidogo,
"Hata mimi nilijifunza, hebu niangalie mimi ninavyofanya nawewe ujaribu"
Alizungumza jamaa yule na kumfanya Junior kuangalia kwa makini, ndani ya dakika kadhaa Junia alikuwa ameshajua na kuanza kumsaidia yule jamaa, Mungu si Athumani wala Dossa,, siku hiyo walipata samaki wengi sana hadi yule jamaa akashangaa, Asubuhi wakaenda kukabidhi wale samaki kwa boss wao ambaye naye alishangaa sana kwani mzigo siku hiyo ulikuwa mkubwa sana zaidi ya siku zote, na kwakuwa hapakuwa na wafanyakazi wengi ilikuwa ni rahisi kwa Junior kuajiriwa na kampuni ile iliyokuwa inasimamiwa na mzungu,,,
*****************************
"Ilipita wiki moja Junior tayri alikuwa mvuvi hodari sana kitendo kilichomfahisha sana boss wake na kuzidi kumsifikia huku akimuahidi kumuongezea mshahara wake, muda wote huo Junior hakuweza kuwasiliana na mama yake ambaye alitafuta hadi akakata tamaa na kuzidi kuchanganyikiwa akajikuta analazwa hospital, mwezi ulipita na Junior kupewa mshahara wake wa kwanza, siku alipopokea mshahara cha kwanza alinunua simu na namba ya kwanza kuisave ilikuwa ni namba ya mama yake,,baada ya kuisave alijaza vocha na kuipigia namba ile, mama yake alipokea kwa kuuliza nani mwenzangu huku sauti yake ikiwa imechoka sana,,
"Ni Mimi mwanao Junior mama"
baada ya sauti ile,alisikia vigeregere vya mama yake na kuwafanya hadi waliokuwa wanamhudumia kushangaa kwani mama Junior alipona ghafla, shangwe zile zilimfanya Junior kuamini kuwa mama yake anampenda mno na ndo pekee anayemtegemea maishani mwake,waliongea mengi sana huku akimtumia mama yake nusu ya mshahara wake"
"Siku zilizidi kwenda huku Junior akiendelea kugawana na mama yake mshahara hivyohivyo,, miaka ilisogea huku Junior akipandishwa kazi na kukabidhiwa ofisi yake kutokana na uaminifu wake kazini na utendaji kazi wake"
"Siku moja Junior akiwa ndani ya gari yake mpya aliyokuwa amenunua akirudi nyumbani kwao, alishangaa akisinamishwa na mzee mmoja aliyekuwa akitembea kwa mguu huku akiwa amepauka sana na kumuomba lift kwani nae alikuwa anaenda Sengerema, Junior hakuwa na kutu moyoni mwake,alimpa lift mzee yule na kuanza kupiga nae story moja mbili,,mzee yule alijikuta akifunguka na kumsimlia maisha aliyopitia;
"Kijana wangu, wakati nikiwa kijana kama wewe nilioa mwanamke ambaye alikuwa mtoto wa kitajili haswa, wazazi wake walitupa kila kitu hadi kazi pia walinipa,nimeishi na mwanamke yule bahati mbaya nikaugua tezi Fulani ya kizazi,madaktari wakaniambia sitakuwa na uwezo wa kumbebesha mimba mwanamke,, kilichoniuma zaidi ilipita miaka miwili nikaona mke wangu tumbo limejaa,nilipomuuliza akanijibu kwa dharau kuwa hawezi kuishi na mwanaume suluari,kiukweli niliumia sana nikaamua kumuacha ila ndo hivyo sikutoka na kitu kwani mali zote zilikuwa za mwanamke,niliingia mjini na kuanza kutafuta kazi lakini sikupata kazi ya maana zaidi ya kazi ndogondogo za kunipatia chakula,, kwa sasa nimezeeka nimeona nirudi nyumbani nikafie kwenye mashamba ya wazazi wangu kwani hapa nilipo nina kansa pia na siku zangu za kuishi zinahesabika,nani atanizika huko mjini wakati sina ndugu hata mmoja,bora hata ningekuwa na watoto"
alizungumza mzee yule nakumfanya Junior kutokwa na machozi kwani aliikumbuka simulizi ya mama yake,
"ukimya ulitawala kwa muda hatimae Junior akafanikiwa kufika mbele ya nyumba fulani ambayo ndo kwanza ilikuwa imekamilika, alisimamisha gari na kushuka, wakati huo mama yake alikuwa jikoni, alipomuona mwanae alikimbia kwa furaha na kumkumbatia huku akishangaa gari ilivyokuwa inang'aa, wakati anashangaa ile gari mara aliona mtu akishuka,,,
"karibu mzee huyu ndo mama yangu"
alizungumza Junior ila alishangaa mzee yule akiwa amemkodolea macho mama junior wakati huo mama junior nae akiwa amemtolea macho mzee yule
"Junior baba yako huyooooo"
alipiga kelele mama junior wakati huo yule mzee alimwangalia mama Junior
"Sarah huyu ndo mwanangu,nisamehee mama"
baada ya kutamka maneno yale yule mzee alianguka hapohapo, Junior aliwahi akambeba na kumuingiza ndani ya gari na kumpeleka hospital, alikaa nje na mama yake wakiwa na hamu ya kujua maendeleo ya baba yake ambaye siku zote alikuwa anatamani kumfaham, baada ya muda waliitwa na dokta,,,,
"Kwanza niwape pole, kiukweli mgonjwa wenu hatuko naye tena duniani kwani ameugua kansa kwa muda mrefu sana ambayo imeathiri mapafu,bora mngemuwahisha ingesaidia"
Junior alilia sana baada ya majibu Yale, siku ya kwanza kumfahamu baba yake,ndo siku baba yake anafariki,,,,,,,,
_____Nini umejifunza hapa?
MWISHO
0 comments:
Post a Comment