SIMULIZI FUPI: USIKIVU NI TIJA
Bwana Makalanga ni kijana anayependa sana kujituma katika kile alichokuwa anakifanya na hii ndo siri kubwa ya mafanikio yake. Bwana Makalanga kipindi alipokuwa anasoma alimuomba sana Mwenyezi ili amjalie apate kazi nzuri na hatimaye mke mwema mara baada ya kumaliza masomo yake.
Bwana Makalanga mara baada ya kumaliza elimu ya chuo kikuu alifanikiwa kupata kazi katika moja ya kampuni ya mitandao ya simu hapa nchini kama msimamizi wa masoko. Baada ya mwaka mmoja maisha ya upweke yaani ya kukaa peke yake bila msaidizi aliyashindwa na hivyo akaanza kutafuta mke ili aweze kusaidiana katika mambo yake amabayo yeye alihisi anahitaji msaada.
Mungu ni mwema kila wakati, bwana Makalanga alifanikiwa kupata mwanamke ambaye baadae alifunga naye ndoa na baada ya muda walipata watoto wawili,wote wakiwa wakiume.Mke wa Makalanga naye alikuwa ni mfanyakazi katika kampuni moja inahusika na uchimbaji na ununuaji wa madini, hivyo kwa kuwa walifanikiwa kununua gari kila siku asubuhi walikuwa wanatoka pamoja nyumbani kwenda kazini kwa kutumia huo usafiri wao.
Mke wa bwana Makalanaga alikuwa anapenda sana kudeka,yaani kila wakati alipenda kumuona mumewe akiwa anamkumbatia ,anamlisha na hata kumuogesha,japo haikuwa rahisi sana kwa bwana Makalanga kuyatimiza hayo yote ila kila wakati alijitahidi kumfanya mkewe awe mwenye tabasamu na furaha wakati wote.
Mrs Makalanga hakuishia hapo,zaidi na zaidi alipenda sana kufunguliwa mlango wa gari na mumewe lakini kwa upande wa bwana Makalanga hakuona umuhimu wowote wa yeye kumfungulia mlango wa gari mke wake ilihari mkewe ana mikono ya kumwezesha kufungua mlango mwenyewe,hivyo bwana Makalanga aliona ni kama usumbufu tu. Mke wa bwana Makalanga wala hakuchoka kumwimiza mumewe jinsi gani anavyojisiksia fahari akiafunguliwa malango wa gari wakati wa kuingia na kutoka ila hasa alipenda sana kufunguliwa na mumewe pindi wanaporejea kutoka kazini lakini bado bwana makalanga wala hakulitimiza hilo na aliona ni kama mambo ya kitoto na ya kuapoteza muda tu.
Siku moja muda mfupi baada ya kumwacha mkewe kazini,majira ya asubuhi bwana makalanga alipata simu ya
kushtusha kwani aliambiwa kuwa mkewe amepata ajari akiwa anavuka barabara na kufariki papopapo, bwana Makalanga aliumia sana sana kwani upendo wake kwa mkewe ni mkubwa sana,wafanyakazi wenzake walimfariji kuwa hiyo ni kazi ya Mungu hivyo yampasa kuvumilia kwani hakuna njia nyingine na hata akilia haitasaidia kumfanya mkewe kuwa hai tena.
Siku ya mazishi ilipofika,mwili wa marehemu uliletwa kutoka hospitali kwa kutumia gari la hospitali ambayo mwili wake ulihifadhiwa,ndugu na jamaa walimtaka bwana Makalanga kufungua mlango wa gari ili mkewe atoke na aingizwe kwenye jeneza teyari kwa mazashi, baada ya kuambiwa hivyo bwana makalanga alilia sana kwa uchungu mkubwa sana kiasi cha watu wote kumshangaa kwa nini alilia sana kipindi anaufungua mlango wa gari ili kuutoa mwili wa marehemu.
Baada ya mazishi,bwana Makalanga aliamua kuwaeleza ndugu na jamaa kwa nini alilia sana kipindi anaufungua mlango,aliwaambia alimkumbuka sana mkewe kipindi cha uhai wake alivyokuwa akimwambia amfungulie mlango akiwa hai lakini hakufanya hivyo na matokeo yake amekuja kufanya hivyo kipindi akiwa amekufa teyari.bwana Makalanga alijilaumu sana kwa nini hakumskiliza mkewe hata kwa siku moja tu, lakini lawama zake hazikuwa na nafasi tena wakati huo .
Bwana Makalanga ni kijana anayependa sana kujituma katika kile alichokuwa anakifanya na hii ndo siri kubwa ya mafanikio yake. Bwana Makalanga kipindi alipokuwa anasoma alimuomba sana Mwenyezi ili amjalie apate kazi nzuri na hatimaye mke mwema mara baada ya kumaliza masomo yake.
Bwana Makalanga mara baada ya kumaliza elimu ya chuo kikuu alifanikiwa kupata kazi katika moja ya kampuni ya mitandao ya simu hapa nchini kama msimamizi wa masoko. Baada ya mwaka mmoja maisha ya upweke yaani ya kukaa peke yake bila msaidizi aliyashindwa na hivyo akaanza kutafuta mke ili aweze kusaidiana katika mambo yake amabayo yeye alihisi anahitaji msaada.
Mungu ni mwema kila wakati, bwana Makalanga alifanikiwa kupata mwanamke ambaye baadae alifunga naye ndoa na baada ya muda walipata watoto wawili,wote wakiwa wakiume.Mke wa Makalanga naye alikuwa ni mfanyakazi katika kampuni moja inahusika na uchimbaji na ununuaji wa madini, hivyo kwa kuwa walifanikiwa kununua gari kila siku asubuhi walikuwa wanatoka pamoja nyumbani kwenda kazini kwa kutumia huo usafiri wao.
Mke wa bwana Makalanaga alikuwa anapenda sana kudeka,yaani kila wakati alipenda kumuona mumewe akiwa anamkumbatia ,anamlisha na hata kumuogesha,japo haikuwa rahisi sana kwa bwana Makalanga kuyatimiza hayo yote ila kila wakati alijitahidi kumfanya mkewe awe mwenye tabasamu na furaha wakati wote.
Mrs Makalanga hakuishia hapo,zaidi na zaidi alipenda sana kufunguliwa mlango wa gari na mumewe lakini kwa upande wa bwana Makalanga hakuona umuhimu wowote wa yeye kumfungulia mlango wa gari mke wake ilihari mkewe ana mikono ya kumwezesha kufungua mlango mwenyewe,hivyo bwana Makalanga aliona ni kama usumbufu tu. Mke wa bwana Makalanga wala hakuchoka kumwimiza mumewe jinsi gani anavyojisiksia fahari akiafunguliwa malango wa gari wakati wa kuingia na kutoka ila hasa alipenda sana kufunguliwa na mumewe pindi wanaporejea kutoka kazini lakini bado bwana makalanga wala hakulitimiza hilo na aliona ni kama mambo ya kitoto na ya kuapoteza muda tu.
Siku moja muda mfupi baada ya kumwacha mkewe kazini,majira ya asubuhi bwana makalanga alipata simu ya
kushtusha kwani aliambiwa kuwa mkewe amepata ajari akiwa anavuka barabara na kufariki papopapo, bwana Makalanga aliumia sana sana kwani upendo wake kwa mkewe ni mkubwa sana,wafanyakazi wenzake walimfariji kuwa hiyo ni kazi ya Mungu hivyo yampasa kuvumilia kwani hakuna njia nyingine na hata akilia haitasaidia kumfanya mkewe kuwa hai tena.
Siku ya mazishi ilipofika,mwili wa marehemu uliletwa kutoka hospitali kwa kutumia gari la hospitali ambayo mwili wake ulihifadhiwa,ndugu na jamaa walimtaka bwana Makalanga kufungua mlango wa gari ili mkewe atoke na aingizwe kwenye jeneza teyari kwa mazashi, baada ya kuambiwa hivyo bwana makalanga alilia sana kwa uchungu mkubwa sana kiasi cha watu wote kumshangaa kwa nini alilia sana kipindi anaufungua mlango wa gari ili kuutoa mwili wa marehemu.
Baada ya mazishi,bwana Makalanga aliamua kuwaeleza ndugu na jamaa kwa nini alilia sana kipindi anaufungua mlango,aliwaambia alimkumbuka sana mkewe kipindi cha uhai wake alivyokuwa akimwambia amfungulie mlango akiwa hai lakini hakufanya hivyo na matokeo yake amekuja kufanya hivyo kipindi akiwa amekufa teyari.bwana Makalanga alijilaumu sana kwa nini hakumskiliza mkewe hata kwa siku moja tu, lakini lawama zake hazikuwa na nafasi tena wakati huo .
MWISHO.
Je umejifunza kitu? kama ndio usiache kumwambia mwenzako kuwa na tabia ya usikivu, kwani kitu kikishatokea hauwezi tena kurudisha muda nyuma ili usikie na kisitokee tena.
0 comments:
Post a Comment