MAUTI YALIBISHA MLANGONI
Daktari Mogiri alifungua mlango polepole na kutoka nje. Alinikuta nimeketi kwa fomu ndefu hapo nje ya wodi nikisubiri. Nilikuwa nimejishika tama na kuzama katika luja ya mawazo. Ni kweli kwamba mshika tama huwa analo moyoni.nilimwangalia kwa macho ya atiati nikitazamiakusikia mengi kumhusu mke wangu Zuhura. Sikujua kilichomtendekea tangu aingizwe mle ndani ya chumba cha upasuaji, masaa matano yaliyopita. Kumbe kweli usilolijua ni kama usiku wa manane.
Akilini mwangu, yaliyotendeka yalikuwa yangali mbichi mno. Nilitoka kazini mapema alasiri hiyo na kurudi nyumbani kwani sikuwa na kazi nyingi ya kufanya. Nikafululiza hadi mlangoni na kubisha bila kupata jibu.wanenao husema kuwa kimya kingi kina mshindo. Nilifungua mlango polepole na kuingia ili kugundua kilichonisubiri. Lo! Ukistaajabu ya musa utayaona ya firauni.
Zuhura alikuwa kalala sakafuni, akigaaga na kufurukuta kwa uchungu na kutoa sauti ya maumivu. Aliye na macho haambiwi tazama. Nilielewa fika kuwasiku zake za kujifungua zilikuwa zimewadia. Kasha akajikazana kutamka,
“Nisaidie jamani.” Kisha akanyamaa ghafla na kuendelea kufurukuta. Fimbo ya mbali haiui nyoki kwa hivyo, niliwaita majirani walionipa usaidizi wa kutafuta rukwama ili kumpeleka hospitalini. Ilikuwa nadra na adimu kama wali wa daku kuona magari katika sehemu tuliyoishi. Sehemu ya Ngomani. Kama wakaazi wa pale, tulizoea maisha hayo na haikuwa ajabu kumwona akipanda au kuabiri ‘gari’ letu- rukwama. tulimpeleka kwa zahanati ya kipekee hapo mjini na kupata kuwa muuguzi hakuwepo. Nikawa nimechanganyikiwa nisijue la kufanya jirani mmoja aliposhauri tumkimbize Zuhura katika hospitali ya wilaya.
Hospitali ya Afueni ilijulikana kote kwa kuwa ya bei ghali. Lakini nilishawishika na kukubali kwani maisha ya Zuhura ilikuwa muhimu kuliko pesa. Tukaandamana hadi kule. Hisia za uchovu na kutamauka tayari zilianza kuninyemelea nikawa nafuata wenzangu tu kama bendera inavyofuata upepo au maji inavyofuata mkondo. Moyo wangu ulijaa ukunjufu kwa ukarimu walionionyesha.
Nikawa nimeketi hapo nikisubiri matokeo ya daktari waliokuwa wakimhudumia. Takribani miaka mine sasa tangu tufunge ndoa, Zuhura alibaki tasa asiweze kupata motto hata mmoja. Mara nyingi nilimsikia akimlilia Muumba wake na kusali. Hatimaye maombi yake yalijibiwa na sasa tulikuwa tukitarajia mwana wetu wa kwanza. Tayari nilikuwa na cheche za matumaini. Penye nia pana njia eti. Hata nikakisia kuwa atakuwa msichana na tungemwita Zawadi. Pengine kama ishara kuwa Maulana alitupa zawadi baada ya miaka. Nilisahau kabisa onyo la wahenga eti usikate kanzu kabla motto hajazaliwa.
Daktari Mogiri akanisongelea na tukaanza majadiliano. Mazungumzo ya kiume kama alivyoyataja. Mara kwa mara niliwaona wauguzi wakipitapita kushoto-kulia wakiendelea na shughuli zao. Daktari alikuwa amemaliza kazi yake muhimu mle ndani.
“Unatarajia mtoto wa jinsia ipi? Mbona? Mtamwita nani? Utampa Zuhura zawadi gain kwa kazi aliyofanya?” aliniuliza maswali chungu nzima. Maswali yenyewe yakatuongoza katika ulimwengu wa gumzo. Tukazungumza na kupitiza wakati bila hata kugundua. Hata chembechembe za wasiwasi nilizokuwa nazo zikanitoka kabisa. Nikajihisi huru, kiumbe mpya na nikavaa piku la tabasamu.
Ndipo sasa daktari akaamua kunipasulia mbarika hatimaye. Akanidokezea kuwa Zuhura alikuwa amejifungua motto wa kiume mwenye buheri wa afya. Singejizuia tena.licha ya kuwa usiku ulikuwa umeingia, nilirukaruka kwa furaha kupindukia ungedhani mwenda wazimu. Nikatamani majirani wote waliomleta Zuhura wangalikuwepo lakini walikuwa washarudi makwao kushughulikia jamii zao. Nikaanza kuwazia jina la motto wetu nikiwa katika hali ya kurukaruka bado.
“Tutamwita Bahati” Nilisema kwa nguvu huku nimemkumbatia daktari kwa furaha macho yangu nikiwa nimeyafumba.
Daktari alikuwa akinitazama tu kwa wakati wote huo pasi na la kusema. Lakini nilipoanza kuuelekea mlango wa chumba alimolazwa mke wangu, alinisitisha na kunizuia. Akaniomba kusubiri lakini furaha iliyonijaa ikanifanya kuwa kiziwi. Nikajitia pamba masikioni nisisikie la mwadhini wala la mteka maji msikitini.
Akanivuta kando kidogo na kunidokezea kuwa Zuhura mwenyewe alifuja na kupoteza damu nyingi hivyo basi asingeweza kuishi! Kwa kifupi, aliniambia kuwa mke wangu alikuwa amea…sikuyaamini macho na masikio yangu. Maneno hayo yalinifanya kiuwa chakaramu zaidi. Yalinikata maini, yakanikera na kunikereketa ajabu. Uso wangu uliokuwa na furaha ulibadilika ghafla na kufinga. Kwa nguvu kama za tembo na hasira za mkizi, niliuendea ule mlango bila kumjali yeyote wala chochote. Alinifuata na kujaribu kunivuta nyuma huku akiniliwaza. Juhudi zake zikangonga mwamba.
Sikujua kuwa daktari ni watu wenye vipawa vha kuwapumbaza watu namna hiyo! Kwa muda wote huo, daktari alikuwa amejua ukweli na kunificha kwa kunishirikisha katika mazungumzo. Pengine hayo ni baadhi ya mafunzo wanayopewa wanaposomea fani ya udaktari lakini ubunifu wa ya Mogiri ulishinda wote. Niliajabia ubunifu wake!
Niliingia kwa fujo na rabsha kama mfungwa aliyeachiliwa huru. Wauguzi wakashtuka na kujaribu kunizuia. Daktari akaingia na kuagiza nionyeshwe mtoto. Nikaelekezwa hadi alikokuwa. Mtanashati ajabu na mwenye afya ungedhani kutoka mbinguni. Alilala kwa utulivu asijue mamake alikokuwa. Laiti angejua. Lakini kuonyeshwa mtoto haikunisaidia wala kinutuliza. Nani angekilisha,akivishe na kukilinda siku zote? Unyama upi huo kuingizwa katika ulimwengu na kuachwa na mwenyeji wako hata kabla ya kumwona ana kwa ana? Nilijihurumia, nikamhurumia malaika wa Mungu. Machozi yakanidondoka kama mtoto na nikayaacha kumwagika bila aibu.
Kwa mwongozo wa daktari, nilifululiza hadi alikolazwa Zuhura. Msichana mrembo aliyeumbwa akaumbika alikuwa amelala kwa upole na utulivu asijue hata wakati wa kuamka. Alikuwa amefunikwa vizuri hata usingedhani ni maiti. Ikanifanya kutoamini na kuanza kumwamsha. “Zuhura, amka umwone Bahati mwana wetu.”
Akawa haoni, hasemezi,hatikisiki. Kimya kikajiri. Niliinama kando yake na kumtikisa tena mara hii kwa nguvu machozi zaidi yakinitoka. Nikamshauri ainuke twende kwetu tusherehekee kuzaliwa kwa mtoto wetu. “Zuhura” niliita mara ya mwisho kwa nguvu na pumzi ikaniishia.
Sauti nyororo ya Zuhura aliyekuwa amelala kando yangu usiku wote ilinigutusha kutoka usingizini ikinijuza kuwa kumekucha. Miale ya jua nayo ilikuwa imeshachomoza nje. Furaha iliyoje kupata kuwa hiyo ilikuwa ndoto ya ajabu.
0 comments:
Post a Comment